Jamaa alikuwa na kesi nzito ya mauaji, ikafikia wakati wa kutoa - TopicsExpress



          

Jamaa alikuwa na kesi nzito ya mauaji, ikafikia wakati wa kutoa hukumu akahisi wazee wa baraza watamuona ana hatiana anaweza akanyongwa, basi akampata mzee mmoja wa baraza akamhonga ili ashawishi wenzie wasimpate na kosa la mauaji ya kukusudia maana atanyongwa, ila japo liwe kosa la mauaji bila kukusudia ili afungwe tu. Kweli baada ya siku tatu wazee wa baraza wakakubaliana kuwa jamaa aliua bila kukusudia, Jaji akampa adhabu ya kifungo cha miaka saba, akashukuru. Alipopata nafasi ya kuongea na mzee aliyemhonga; MFUNGWA: Mzee nashukuru sana nategemea sikukupa kazi nzito MZEE: Loh ilikuwa kazi nzito sana, wenzangu wote walikuwa wameona huna hatia hivyo kuwabembeleza wakubali kuwa umeua bila kukusudia ilikuwa ngumu sana.
Posted on: Sun, 06 Oct 2013 21:04:29 +0000

Trending Topics



Recently Viewed Topics




© 2015