Maisha yalizidi kuwa magumu na sikuwa na jinsi zaidi ya kusafiri - TopicsExpress



          

Maisha yalizidi kuwa magumu na sikuwa na jinsi zaidi ya kusafiri kutoka Moshi na kwenda kusini mwa tanzania kusaka maisha. Tangu mzee afariki maisha yalikuwa magumu kwetu na kama ujuavyo maisha ya mama zetu wa kiafrika, baba zetu waliwasahau katika kuwaweka karibu na utafutaji wa fedha wao walibaki nyumbani sasa fikiri mzee kafariki na tuko watoto sita tutaishije? Mama yangu nilimwahidi lazima kabla ya uzee wake au kifo kumchukua lazima afurahie matunda yake kupitia mimi na alikuwa na furaha kila siku kusia maneno hayo toka kwangu. Nilifika mkoa huo kusini mwa Tanzania na nilishangazwa kuona mtoto mdogo kuliko mimi ana utajiri wa kutisha.... duuuh mate yalikuwa yakinidondoka hasa ukizingatia sikuwa na kipato cha kuanza biashara yangu wala elimu kubwa ikabidi yule kijana aniajiri katika shamba lake la chai na mimi nikawa msimamizi pale. Baada ya mwaka mmoja wa kuzoea pale huku nikifanikiwa kupata hela kidogo na kumtumia mama yangu niaanza kuona mambo sio mabaya sana ila nakumbuka kuna jamaa yangu mmoja aliyekuja nyuma yangu ghafla nikaanza kusikia kuwa jamaa kashapata utajiri maana mara ananunua viwanja anajenga hotel na fedha kibao. Ndipo nikaambiwa kuwa mimi tuu ndio fala wenzangu wote huenda kijiji jirani ambako kuna mzee mmoja ambaye yeye huwapa vijana utajiri. Kwa siri nikajiandaa na nikamtembelea yule mganga na hakuniambia nimpe hela alisema ananipa dawa nikishapata fedha niende kumshukuru. Ila akasema nilale pale kwani kuna mtihani nitaufanya kabla ya kwenda kuitumia ile dawa na kuniuliza kama sio mwoga na nipo jasiri. Jioni ile alinipa mkuki na kuniambia nipite uchochoro mmoja na kuwa nitakutana na kitu cha kutisha nisikiogope na nikienda hatua chache nitakutana na cha pili wala nisiogope pia ila cha tatu tu kikitokea niurushe mmkuki na kukiua pale pale kisha nirudi haraka kwa mganga. Nikauchukua mkuki na kuanza kuufuta ule uchochoro, hatua chache tuu nikaona bonge la nyoka likinijia kwa mbele nikajikaza nae akasepa zake wakati huo mkojo na jasho ninaninyanyasa, hatua chache mbele akatokea simba wa ajabu nae ananifuata nikajikaza akapita na kupotea ile najiandaa kuuweka mkuki sawa ili kile cha tatu nikipe mkuki mara naona mama yangu ndio anakuja, niliutupa mkuki na kwenda kwa mganga na kumwambia aisee nimeshindwa mimi plz nipe jaribio jingine hili la mama sio. Mganga akachukia na kunipa ndoano pamoja na fimbo yake na kusema nenda hapo mtoni iinginze hii kwenye maji kitu ukihiisi kama samaki kimenasa wewe ibebe ndoano na bila kuangalia nileteee. Nikafanya hivyo na ile ndoano ilivyokuwa nzito nikainyanyua na kuiweka mgongoni na kisha kuondoka ila kabla sijafika kwa mganga nikasema ngoja nigeuke na kuangalia ni nini, duuuh kumbe tena nimemvua mama yangu. Nikakimbia na kumwambia mganga mie nimeshindwa huku nikiwa nimechanganyikiwa akanipa dawa na kusema kimbia sana tafuta usafiri uanze kwenda moshi ukifika pale mmwagie mama yako maji haya.kwani muda huu atakuwa kaanguka na wamemkimbiza hospitali maana utajiri huu ni lazima mama yako au ndugu afe ili upate. Niliunga unga usafiri na siku ya pili jioni nikawa moshi, kweli wakaniambia mama alianguka tu jana jioni na hawajui kuna nini, nikamwamgia dawa ile akapona na ndio nikawasimulia kilichotokea. Wakanisema sana sana na sasa nimeokoka na nimepata utajiri kwa njia ya halali na ninakoma na nimekoma kuupenda utajiri wa mkato……………. Sitaisahau siku hii ambayo kidogo nimpoteze mama yangu kwa tama za utajiri wa mkato
Posted on: Sun, 17 Nov 2013 10:18:18 +0000

Trending Topics



"> g “In the last day, that great day of the feast, Jesus stood
❖ Posterior Cerebral Artery : #UME_Neuroanatomy At the level
URO Parts 06A 121 132Q Cooling Hose Flange with O-Ring Want to

Recently Viewed Topics




© 2015