Katika Amka na BBC asubuhi hii .... Umoja wa mataifa wamhusisha rais wa Syria Bashar al Assad na uhalifu wa kivita na uhalifu dhidi ya binadamu, wachunguzi wa umoja huo wanataka afikishwe mbele ya mahakama ya ICC. Rais wa jamhuri ya kidemokrasia ya Congo Joseph Kabila akubali kurejea kwenye meza ya mazungumzo ya amani na kundi la waasi la M23 mjini Kampala. Na waandishi wa habari pamoja na wakereketwa wa haki za kimsingi nchini Kenya wapanga maandamano kupinga mapendekezo mapya yaliyotolewa na rais wa taifa hilo kudhibiti vyombo vya habari.
Posted on: Tue, 03 Dec 2013 02:41:52 +0000
Trending Topics
Recently Viewed Topics
© 2015