Kuna jamaa alilala juu ya mti kumbe chini ya mti ule wachawi - TopicsExpress



          

Kuna jamaa alilala juu ya mti kumbe chini ya mti ule wachawi wanakutana,walipofika wakaanza kujitambulisha mimi mchawi kutoka Sumbawanga mimi mchawi kutoka Tanga, mimi kutoka Naigeria, mimi kutoka Congo. Jamaa anawasikiliza tu akatokea mmoja akasema mimi mchawi kutoka Afghanistani,, jamaa akasema mmh huyu atajilipua sasa ivi hawachelewi hawa. Tutakufa sote, kwa hofu akaruka puu chini. Nae akajitambulisha mimi ni mchawi toka MBINGUNI. Wachawi wote mbioo
Posted on: Tue, 19 Nov 2013 05:24:58 +0000

Trending Topics



Recently Viewed Topics




© 2015