Mabudha wenye misimamo mikali wanaendelea kuwatesa na kuwanyanyasa - TopicsExpress



          

Mabudha wenye misimamo mikali wanaendelea kuwatesa na kuwanyanyasa Waislamu wa Myanmar huku serikali ya nchi hiyo ya kusini mashariki mwa Asia ikionekana kuwatelekeza Waislamu hao. Leo Jumapili vyombo vya habari vimeripoti kuwa, makundi ya Mabudha wenye chuki za kidini wamevamia nyumba tano za Waislamu katika mji wa Kyaung Gone, yapata kilomita 50, kaskazini magharibi mwa mji mkuu Yangon na kuzichoma moto nyumba hizo. Vyombo vya habari vya serikali vimedai kuwa polisi wamewatia mbaroni Mabudha 40 kwa kushambulia nyumba za Waislamu. Polisi wanasema kuwa, tarehe 2 mwezi huu wa Oktoba, Waislamu watano wakiwemo wanaume wanne na mwanamke mmoja waliuliwa kikatili katika kijiji cha Thabyuchaing baada ya mamia ya Mabudha wenye misimamo mikali kuvamia kijiji hicho. Wiki iliyopita pia, bikizee mmoja aliuliwa kwenye eneo la Thandwe, katika jimbo la Rakhine baada ya zaidi ya Mabudha 700 kumiminika mitaani kuwasaka Waislamu na kuchoma moto nyumba zao. Mashirika ya haki za binaadamu yanailamumu serikali ya Myanmar kwa kudharau wajibu wake wa kuwalinda Waislamu.
Posted on: Sun, 06 Oct 2013 17:33:00 +0000

Trending Topics



Recently Viewed Topics




© 2015