SHINIKIZO LA DAMU HUSABABISHWA NA NINI? AINA YA KWANZA: Asilimia - TopicsExpress



          

SHINIKIZO LA DAMU HUSABABISHWA NA NINI? AINA YA KWANZA: Asilimia 90-95 sababu huwa hazijulikani na kitaalamu huitwa primary or essential hypertension. Ingawa vitu vifuatavyo vimehusishwa kupelekea kupata aina hii ya shinikizo la damu. Navyo ni: Uvutaji sigara Unene (visceral obesity) Unywaji wa pombe Upungufu wa madini ya potassium Upungufu wa vitamin D Kurithi Umri mkubwa Chumvi na madini ya sodium kwa ujumla Ongezeko la kemikali kwenye figo (renin) Kushindwa kufanyakazi kwa kichocheo kiitwacho insulin AINA YA PILI: Asilimia 5 huwa na sababu dhahiri zinazopelekea kupata aina hii ya shinikizo la damu na huitwa kitaalamu secondary hypertension. Na sababu hizi ni: Hali ya kukosa hewa usingizini (sleep Apnea) Kasoro ya kuzaliwa nayo katika mshipa mkubwa wa damu (Coarctation of Aorta) Saratani za figo (wilm’s tumor, renal cell carcinoma) Saratani ya tezi iliyo juu ya figo (pheochromocytoma) Ujauzito – wapo wakina mama wajawazito ambao hupata shinikizo la damu na huwa hatarini kupata kifafa cha mimba (eclampsia) Magonjwa ya figo (renal artery stenosis, glomerulonephritis DALILI ZAKE Mara Nyingi Huwa Hamna Dalili Zozote, Na Kama Zikiwepo Mgonjwa Huwa Na Dalili Zifuatazo: Uchovu Maumivu Ya Kichwa Kuhisi Mapigo Ya Moyo Kwenda Haraka Kichefuchefu Kutapika Damu Kutoka Puani Kutoweza Kuona Vizuri (Blurred Vision) Kusikia Kelele Masikioni Na Mara Chache Kuchanganyikiwa Kupoteza Hamu Ya Tendo La Ndoa Na Upungufu Wa Nguvu Za Kiume MADHARA YANAYOWEZA KUELETWA NA SHINIKIZO LA DAMU Kiharusi Moyo Kushindwa Kufanya Kazi ( Congestive Heart Failure) Madhara Katika Mshipa Mkubwa Wa Damu Ambapo Ukuta Wa Ndani Huchanika Na Damu Hukusanyika Katika Ukuta Wa Mshipa Huo(aortic Dissection) Magonjwa Ya Mishipa Ya Damu Kushindwa Kuona Athari Katika Ubongo Kupungua Nguvu Za Kiume JINSI YA KUZUIA SHINIKIZO LA DAMU Chakula cha afya kisicho na mafuta mengi na chenye madini ya potassium kitaalamu kinaitwa DASH diet (dietary approaches to stop hypertension) Mazoezi mara kwa mara- angalau nusu saa kwa siku Kwa wavutaji sigara kuacha kuvuta sigara Punguza au kama unaweza acha unywaji wa pombe ( kwa wanaume angalau bia 2 kwa siku na wanawake bia 1) Punguza utumiaji wa chumvi hasa ya kuongeza mezani (usitumie zaidi ya gramu 1.5) Punguza msongo mawazo Hakikisha unakuwa kwenye uzito wa afya, kama uko kwenye uzito wa hatari fanya mpango wa kupunguza uzito. Matumizi ya mafuta ya samaki husaidia kupunguza shinikizo la damu, kwa wenye shinikizo la damu
Posted on: Sun, 24 Nov 2013 11:00:01 +0000

Trending Topics



Recently Viewed Topics




© 2015