Tunawaomba Watanzania, wanachama na viongozi wetu wasife moyo, bali waendelee kukiunga mkono chama chao cha ukombozi, CHADEMA. Tunawaomba Watanzania, wanachama na viongozi wetu waendelee kulilinda tumaini lao pekee la mabadiliko ya kisiasa, kiuchumi na kijamii katika nchi yetu. Badala ya kukatishwa tamaa, kila mmoja wetu aongeze bidii maradufu ili kuwashinda wale wanaotaka kuleta majanga katika Chama chetu na kwa Taifa letu. ------------------------------------------ FREEMAN AIKAELI MBOWE (MB) - MWENYEKITI, TAIFA ------------------------------------------ WILBROD PETER SLAA KATIBU MKUU
Posted on: Fri, 22 Nov 2013 21:37:53 +0000
Trending Topics
Recently Viewed Topics
© 2015